Header Ads

Kamati ya Maandalizi ya Tuzo za Filamu Tanzania yashauriwa kutangaza Tasnia ya Filamu kimataifa

 Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo (Kulia) akifungua kikao kati ya wajumbe kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo pamoja na Kamati ya maandalizi ya Tuzo za TAFA leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel.
 Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akizungumza na wadau wa filamu waliofika katika Ofisi za Wizara hiyo kuwasilisha taarifa ya maandalizi ya Tuzo za TAFA nchini itakayofanyika tarehe 23 Mei mwaka huu. Kulia ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo
 Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tuzo za TAFA Bibi. Caroline Gachara Gul (kulia) akiwasilisha taarifa ya maandalizi ya Tuzo za TAFA nchini kwa Uongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo pamoja na watendaji kutoka Bodi ya Filamu nchini leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mjumbe wa kamati hiyo Bibi. Siima Rubibira.
 Wajumbe kutoka Kamati ya Maandalizi ya Tuzo za TAFA pamoja na maafisa wanaosimamia Filamu nchini kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakimsikiliza kwa makini mjumbe aliyekua akichangia (hayupo pichani) wakati wa kuwasilisha taarifa ya maandalizi ya Tuzo hizo kwa uongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
 Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania Bw. Saimon Mwakifwamba (kushoto) akichangia wakati wa kuwasilisha taarifa ya maandalizi ya Tuzo za TAFA nchini kwa uongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo pamoja na watendaji kutoka Bodi ya Filamu nchini leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni mjumbe wa kamati hiyo Bw. John Kalage.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Mchezo Prof. Elisante Ole Gabriel (waliokaa katikati), Mkurugenzi Idara ya Utamaduni Prof Elimas Mwansoko (wapili kushoto), na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo (wapili kulia) katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Tuzo za TAFA na watendaji wanaosimamia shughuli za filamu nchini. Picha na: Genofeva Matemu - Maelezo.

No comments:

Powered by Blogger.