Header Ads

WAZIRI LUKUVI AFUNGUA NYUMBA ZA NHC MRARA BABATI


1
Sehemu ya nyumba 40 za gharama nafuu zilizojengwa na NHC eneo la Mrara Babati mkoani Manyara ambazo zilifumguliwa rasmi na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Vangimembe Lukuvi.
.....................................
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi amehitimisha ziara yake ya kutatua migogoro ya Ardhi katika mikoa ya Mwanza, Arusha na Manyara na ameweza pia kuweka jiwe la msingi mradi wa nyumba za gharama nafuu Buswelu Mwanza na kufungua nyumba za aina hiyo zilizojengwa na NHC katika eneo la Longido Arusha na Mrara Babati. Picha za ufunguzi wa Mradi wa Mrara na Muungano Saguya-Babati
New Picture (1)
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akitoa maelekezo kwa watendaji wake muda mfupi kabla ya ufunguzi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC eneo la Mrara Babati mkoani Manyara
New Picture (2)
Kikundi cha sanaa kikiburudisha halaiki ya wananchi( haiku pichani) iliyohudhuria ufunguzi uliofanywa na Waziri Lukuvi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHCeneo la Mrara Babati mkoani Manyara.
New Picture (3)
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akionyeshwa mipaka ya eneo linalomilikiwa na NHC na Msimamizi wa Mradi wa NHC Mrara Babati Bi Linda Kasilima baada Mkurugenzi Mkuu kubaini kuwepo kwa uvamizi wa baadhi ya viwanja vya Shirika. Kufuatia hali hiyo Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Joel Bendera ameagiza wote waliovamia viwanja hivyo kunyang’anywa mara moja na nyumba zao kuvunjwa bila fidia.
New Picture (4)
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Kyando Mchechu akimpokea Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Vangimembe Lukuvi alipowasili katika mradi wa nyumba za gharama nafuu unaotekelezwa na NHC ambapo aliifungua rasmi baada ya kukamilika. Nyjmba hizo 40 sasa zinauzwa kwa wananchi mbalimbali wa Babati na nje ya Wilaya hiyo wanaohitaji.

No comments:

Powered by Blogger.