Header Ads

Mh Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu alipo zindua magari yalionunuliwa kwa ajili ya kupambana na Ujangili


 Mh Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu akitelemka katika moja ya gari ambalo alilizindua kwa ishara ya kuzindua magari mengine yote yatakayotumika kupambana na ujangili.
  Mh Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu  akielekea kuongea na wanahabari baada ya uzinduzi huo
 Haya ndiyo Magari ambayo yamezinduliwa Rasmi kwa ajili ya kupambana na majangili 
 Mh Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu akizungumza na wanahabari.Picha zote na Maliasili zetu Blog

HII NDIO HOTUBA YAKE KAMILI 


Ndugu Wanahabari:
Katika kutekeleza maazimio ya Bunge, na ahadi  ya serikali kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maliasili, Ardhi na Mazingira, leo nimekamilisha utaratibu wa kuzitoa silaha zilizokuwa  chini ya TRA tangu mwezi wa Novemba mwaka 2012, ili kuzikabidhi kwa wapiganaji katika Hifadhi za Taifa, Mamlaka ya Ngorongoro, na Mapori ya  Akiba kote nchini kwa lengo la kupambana na ujangili. Silaha hizi 500  aina ya AK47 ziligharimu jumla yaSh.427milioni kuzinunua, na leo Wizara  yangu inatoa Shs.212 milioni kwa ajili ya kulipia kodi na ushuru  mbalimbali ili Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA iziruhusu kutolewa.

No comments:

Powered by Blogger.