CCM: ZIARA ZA KINANA ZIMEONYESHA KUZAA MATUNDA
CHAMA Cha
Mapinduzi (CCM) kimesema ziara ambazo zimekuwa zikifanywa na Katibu
Mkuu wake, Abdulrahman Kinana, zimeanza kuzaa matunda hasa upande wa
utatuzi wa kero zinazowakabili wananchi.
Hayo
yamesemwa leo, Novemba 12, 2013, na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi,
Nape Nnauye wakati akitangaza kuanza kwa ziara ya Kinana ya siku 22,
katika mikoa ya mikoa ya Ruvuma na Mbeya itakayoanza, Novemba 15, 2013,
ambayo ni mwendelezo wa ziara za kuimarisha chama, kukagua utekelezaji
wa Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010, kusikiliza kero za wananchi
na kushirikiana nao kuzitafutia ufumbuzi.
Nape
alisema miongoni mwa mafanikio yanayoonekana kutokea ni mwitikio
ulionyeshwa na serikali katika kutekeleza maagizo yaliyotolewa kupitia
ziara zilizopita za Kinana, na vikao vya Chama kuhusu kushughulikiwa kwa
kero au hoja mbalimbali.
Alisema, baadhi ya kero ambazo zimeshuhudiwa zikichukuliwa hatua na serikali ni pamoja na kufufua viwanda nchini.
Nape
alisema baada ya ziara kadhaa za Katibu Mkuu, uchambuzi na vikao kadhaa
vya CCM, Chama kiligundua kuwa viwanda vingi vilivyo binafsishwa
havifanyi kazi kama ilivyokusudiwa na vingine kufungwa kabisa na
kugeuzwamagodauni.
Alisema
pamoja na athari kubwa kwa uchumi wa nch, kufungwa na kutofanya vizuri
kwa viwanda hivyo kumechangia sana tatizo la ajira kuwa kubwa, hivyo
Chama kiliagiza serikali kufanya tathimini ya viwanda vyote vilivyo
binafsishwa na hali yake kwasasa na vile visivyofanya kazi kama
ilivyokusudiwa vichukuliwe na serikali na kutafuta njia sahihi ya
kuvifufua upya.
Nape
alisema, baada ya chama kuagiza kupitia ziara za Kinana na vikao vya
Chama, serikali imechukua hatua kadhaa katika hili, ikiwemo kufanya
tathimini na mapendekezo kadhaa yamewasilishwa na timu iliyoundwa na
serikali kwa serikali kwa ajili ya kufanyia uamuzi na kuchukua hatua.
Alisema,
CCM inatambua kwamba zipo hatua kadhaa ambazo imechukuliwa na serikali
katika jitihada za kufufua viwanda vya kubangua korosho kama sehemu ya
utatuzi wa tatizo la soko na zao la korosho na kwamba na sasa serikali
ipo katika hatua kadhaa za kushughulikia viwanda vingine nchini.
Nape
alisema, kutokana na mwitikio huo, CCM inaipongeza serikali kwa hatua
hizo muhimu za kutekeleza agizo la Chama, ingawa pamoja na pongezi hizo
CCM imeitaka serikali ikamilishe kazi hiyo mapema iwezekanavyo ili nchi
ifaidike na ufufuaji huo wa viwanda nchini.
No comments:
Post a Comment