Header Ads

Matokeo ya Nani Mtani Jembe kuanza kutangazwa leo

Mwenyekiti wa Simba SC, Aden Rage akishangilia na wafanyakazi wa kiwanda cha TBL Mbeya wanaoshabikia Simba baada ya kuibuka washindi katika shindano la kuvuta kamba katika hafla ya kuzindua kampeni ya Nani Mtani Jembe kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho mwishoni mwa wiki jijini Mbeya.
Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe akitambulisha kampeni ya Nani Mtani Jembe kwa wafanyakazi wa TBL Mbeya mwishoni mwa wiki.
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Yanga, Mohammed Bhinda akimkabidhi Nancy Tibanyenda zawadi baada ya timu yake kushinda mchezo wa kuvuta kamba katika hafla ya kuzindua kampeni ya Nani Mtani Jembe kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho mwishoni mwa wiki jijini Mbeya.
Wafanyakazi akinamama wa TBL Mbeya wakishindana kuvuta kamba katika hafla ya kuzindua kampeni ya Nani Mtani Jembe kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho mwishoni mwa wiki jijini Mbeya.


No comments:

Powered by Blogger.