Header Ads



KIONGOZI HUYU AMBAYE  AMECHAGULIWA TENA KUENDELEZA LIBENEKE HILO.


Zuriki, Uswizi - 01/06/2011. Wajumbe wa shirikisho la soka duniani FIFA,wamemchagua tena rais wa shirikisho hilo kushikiria kiti hicho kwa kipindi kingine cha miaka minne.
Wajumbe hao waliweza kumchagua Sepp Blatter kwa wingi wa kura zipatazo 186 kati ya kura 203 zilizo pigwa.
Sepp Blatter, ambaye alikuwa mgombea pekee katika kiti hicho, baada ya mpinzani wake Mohamed bin Hammam kujitoa kutokana na kashfa za rushwa.
Hata hivyo, uchaguzi huo ulifanyika baada ya Uingereza kushindwa kuwashawishi nchi wanachama wa shirikisho hilo kupiga kura ya kutaka uchaguzi huo usimamishwe kwa muda, ili achaguliwe mpinzani dhidi ya Sepp Blatter, lakini matokea ya kura hizo yalipinga maombi ya Uingereza kwa 172 kutaka uchaguzi ufanyike na 17 kuunga mkono Uingereza.
Kuchaguliwa kwa Sepp Blatter, kumeaandamana na misukosuko mingi iliyo ikuta shirikosho hilo baada ya kashfa za rushwa kuandama uongozi mzima wa shirikisho hilo FIFA.
Akiongea baada ya matokeo ya uchaguzi, rais huyo wa FIFA Sepp Blatter alisema "Mimi ni kaptain ambaye naongoza jahazi lililo kumbwa na mawimbi na tuta hakikisha shirikisho la soka litakuwa mairi na kulinda heshima ya mchezo huu, kuweka wazi kila jambo na kuhakikisha matatizo yaliyo tokea hayatotokea tena, na nahaidi kwa baraka za Muumba na uzima atakao nipa basi tuta fanikiwa kuhakikisha shirikisho hili lina kuwa swafi na imara."

No comments:

Powered by Blogger.