Header Ads

MGIMWA AWAKUNA WAZEE NYAMIHUU WAMCHANGIA TSH 100,000 YA FOMU YA UBUNGE


Mbunge wa jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa akishuka katika pikipiki (Boda Boda) akitoka kukagua ujenzi wa zahanati kijiji cha Nyamihuu leo.
Mbunge wa jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa akikabidhi saruji mifuko 60 kwa mwenyekiti wa kijiji cha Nyamihuu Bw Richard Mbembe  kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji kama sehemu ya utekelezaji wa ahadi zake.
Wazee kijiji cha Nyamihuu wakimchangia pesa za fomu Mgimwa kulia.

Na matukiodaimaBlog
WAZEE  wa kijiji cha Nyamihuu kata ya Nzihi wamempongeza mbunge wa jimbo la Kalenga Godfrey Mgimwa kwa kumchangia Tsh 100,000 ya kuchukulia fomu tena ya ubunge baada ya kuwatumikia  vizuri kwa muda wa mwaka mmoja wa ubunge wake .

Wakitoa pongezi hizo leo wakati wa ziara ya mbunge huyo kumalizia ahadi Yake ya Bati 60 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho ,walisema kuwa wamevutiwa na chapakazi wake alioonyesha katika kipindi chake kifupi cha mwaka mmoja.

Akizungumza kwa niaba ya wazee hao na wananchi wa Kijiji cha Nyamihuu Bi shekela Mvela  alisema wamelazimika kuchangishana kila mmoja kiasi cha Tsh 10,000 na kufikisha kiasi hicho cha Tsh 100,000 kama ahsante Yao kwa mbunge huyo.

Hata hivyo walisema imani kubwa ambayo wao wameionyesha kwa mbunge huyo ni wazi ni imani ya wananchi wote wa jimbo hilo ambao wamepata kushuhudia Kazi nzuri iliyofanya na mbunge huyo kijana kwa muda mfupi zaidi ukilinganisha na wabunge waliotangulia ambao walikuwa wakiahidi pasipo kutimiza

Kwa upande wake diwani wa kata ya Nzihi Steven Mhapa mbali ya kumpongeza mbunge huyo kwa utekelezaji wa ahadi zake bado alisema CCM itaendelea kushinda katika jimbo hilo kutokana na utekelezaji mzuri wa ilani uliofanyika.

Kwa upande wake mbunge Mgimwa ambae alipokelewa kwa maandamano ya Boda Boda katika kijiji hicho cha Nyamihuu alisema amefarijika zaidi kwa upendo mkubwa ulioonyeshwa na wananchi hao wa Nyamihuu pia mchango wao wa fedha ya kuchukulia fomu

Alisema kuwa wapo ambao wanaeneza uvumi kuwa hatagombea tena ubunge jambo ambalo si kweli isipo kuwa baada ya bunge kuvunjwa atachukua fomu tena ya ubunge ili kupata kipindi chake cha miaka mitano ya kuwaletea maendeleo wananchi hao wa jimbo la Kalenga .

mbunge Mgimwa alitaja ahadi mbali mbali zilizokuwa zimebaki kata ya Nzihi na kuzitekeleza leo kuwa katika  kijiji cha kipera amekabidhi Tsh 500,000 kwa kikundi cha Umoja PTC, Kwaya ya mtakatifu Thomas Nzihi amekabidhi Tsh milioni 1, kanisa la TAG nzihi Bati 44 ,kijiji cha Nyamihuu mifuko 60 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya kijiji na Kidamali Tsh milioni 1.2 kwa ajili ya ujenzi wa ghala la kijiji.

Alisema dhamila Yake ni kutimiza ahadi zake zote ndani ya siku mbili hizi ili anapogombea tena ubunge asiwe na kiporo cha ahadi.

No comments:

Powered by Blogger.