KAMPUNI YA MABATI YA AFRICAN ALLUMIUM (ALAF), IMEZINDUA MABATI AINA YA ROYAL VERSATILE
Ofisa
Mauzo wa Kampuni ya Mabati ya Alluminium Afrika (Alaf), Yahya Ngoza akizungumza
na mmoja kati ya wateja waliotembelea banda hilo, wakati wa Maonyesho ya 39 ya
Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF), katika Viwanja vya Mwalimu J.K
Nyerere barabara ya Kilwa.
Ofisa
Mauzo wa Kampuni ya Mabati ya Alluminium Afrika (Alaf), Monica Reuben akitoa
maelezo kwa baadhi ya watu waliofika katika banda la kampuni hiyo, wakati wa
Maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF), katika Viwanja
vya Mwalimu J.K Nyerere barabara ya Kilwa.
Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Kampuni ya Mabati
ya African Allumium (Alaf), imezindua mabati mapya aina ya Royal Versatile
ambayo yana uwezo mkubwa wa kuhimili kutu na mazingira mengine ya hali ya hewa
popote nchini.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi wa mabati hayo, Meneja Masoko wa Alaf, Theresia Mmasy
alisema kuwa mabati hayo yamezinduliwa rasmi wakati wa maonyesho ya 39 ya
Biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalimu J.K Nyerere, barabara ya
Kilwa.
Alisema
mabati hayo ambayo yana viwango vya kimataifa na yameanza kuuzwa pia nje ya
nchi, yanamudu mazingira yote ikiwa ni pamoja na ukanda wa Pwani ambako hali ya
hnewa yake ina kiwango kiklubwa cha chumvi.
“Maeneo
mengine ni lazima ujenge na vigae na sio bati kutokana na kiwango kikubwa cha
chumvi katika hewa” alisema na kuongeza kuwa hali hiyo husababisha mara nyingi
kutu katika mabati hivyo kuyasababishia kuharibika katika kipindi kifupi.
Alisema
utalaam na teknolojia iliyotumika katika utengenezaji wa mabati hayo unafanya Tanzania kama Taifa kuwa na eneo la kujivunia
katika sekta ya ujenzi tofauti na siku za nyuma.
“Tuna
bidhaa ambayo inaweza kushindana kimataifa na pia kupanua wigo wa biashara
katika nchi za Afrika Mashariki, Kat8i na Kusini” alisema Mmasy.
Kampuni hiyo
ambayo asilimia kubwa ya hisa zakwe zinamilikiwa na serikali, imetoa punguzo
maalum kwa wateja ambao watanunua mabati hayo wakati wa maonyesho hayo, lengo
likiwa kuchangia pato la Taifa na kusaidia ujenzi wa nyumba bora nchini.
No comments:
Post a Comment