Header Ads

RAY C : SIJAACHA KUTUMIA DOZI YA METHADONE

cb26f-raycccDiva wa muziki wa Bongo Fleva, Ray C  A.K.A kiuno bila mfupa, amekanusha habari zilizogaa mitandaoni na kwenye magazeti ya udaku zinazodai kuwa amekacha kwenda kwenye kituo tiba kinachotoa dawa za Methadone mahususi kwa waathirika wa dawa za kulevya kilichopo katika  hospitali ya Mwananyamala .
Mimi naendelea na Methadone, huu ni mwaka wa pili nakaribia namaliza, kwaiyo naendelea vizuri, kila mwezi kuna ripoti inatoka inaenda kwa mheshimiwa na vipimo vyangu kila mwezi, nafanyiwa vipimo, nafanyiwa counselling…katika wagonjwa ambao  wanaoendelea vizuri na Methadone”, alisema Ray c kwenye mahojiano na hot 255 ya Clouds fm.
Aidha mwanamuziki huyo amesema wanampango wa kuendelea na projekti ya maskani kwa maskani kupitia mradi wake wa Ray C Foundation na wanategemea kwenda mikoani ila kwa sasa wanajaribu kutafuta wadhamini.
”Tunaplan ya kuendelea na projekti ya maskani kwa maskani na tunategemea kwenda mikoani pia ila tunajipanga tuweze kuongea na wadhamini, kwa sababu kwa nguvu zetu sisi wenyewe hatuwezi kuwafikia watanzania wengi, kwaiyo tunachofanya tunajaribu kuongea na mashirika mbalimbali”, alisema Ray C

No comments:

Powered by Blogger.