Header Ads

DKT. KIGODA AZINDUA BODI YA UONGOZI YA CHUO CHA CBE LEO JIJINI DAR ES SALAAM.


 Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Abdallah Kigoda akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Chuo cha CBE na menejimenti ya chuo hicho kabla ya kuzindua rasmi Bodi mpya ya uongozi ya chuo hicho leo.
 Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Abdallah Kigoda (kulia) akimkabidhi mwongozo wa utendaji kazi Mwenyekiti wa Bodi iliyoteuliwa ya uongozi wa Chuo cha Elimu ya Biashara, Prof. Mathew Luhanga (kushoto) leo jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Abdallah Kigoda (katikati) akizungumza jambo na viongozi na wajumbe wa Bodi mpya ya uongozi ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) iliyoteuliwa alipokuwa akitembelea maeneo mbalimbali ya chuo hicho leo jijini Dar es salaam. Kutoka kushoto ni Mkuu wa chuo hicho Prof. Emanuel Mjema akifuatiwa na Makamu Mwenyekiti wa Bodi Prof. Eleuther Mwageni na Prof. Mathew Luhanga ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Uongozi ya CBE (kulia).
 Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Prof. Emanuel Mjema (kushoto) akimwonesha Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Abdallah Kigoda baadhi ya maeneo ya chuo yaliyokuwa yamevamiwa na watu na kujengwa majengo yakiwa wazi baada ya kubomolewa kufuatia uongozi wa chuo hicho kuendelea na juhudi za kuyarudisha maeneo yote yaliyokaliwa kinyume cha sheria chini ya umiliki wa chuo.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Abdallah (katikati)Kigoda akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Uongozi wa Chuo cha CBE na Menejimenti ya CBE leo jijini Dar es salaam. 

 Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Abdallah Kigoda akisalimiana na viongozi na wafanyakazi wa Chuo cha Elimu ya Biashara kampasi ya Dar es salaam alipowasili chuoni hapo kuzindua Bodi mpya ya uongozi ya Chuo hicho leo.Picha na Aron Msigwa- MAELEZO.

No comments:

Powered by Blogger.