Header Ads

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA AMALIZA ZIARA YAKE NEWALA, LEO YUKO TANDAHIMBA

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Newala Kepteni Goerge Mkuchika wakati wa mapokezi wilayani Newala.
 Wafanyakazi wakibangua korosho kwenye kiwanda cha Micronix Newala ambacho kilitembelewa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambaye yupo kwenye ziara ya kujenga na kuimarisha chama mkoani Mtwara
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kuchagua korosho na kuzitenga kutokana na ubora wa madaraja kwenye kiwanda cha Micronix kilichopo Newala mkoani Mtwara.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kulia)akishiriki kusuka nondo pamoja na mbunge wa Jimbo la Newala Kepteni George Mkuchika kwenye ujenzi wa tenk la maji Kilidu wilayani Newala mkoa wa Mtwara.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua kituo cha afya cha Mkwedu wilayani Newala ikiwa sehemu ya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM.
 Jengo la Kituo cha Afya Mkwedu wilaya ya Newala.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Newala kwenye viwanja vya Mahakama ya Mwanzo ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa Serikali lazima itafute namna ya kuhakikisha uzalishaji wa korosho wote unafanyika nchini kwa kujenga viwanda vya kutosha vya korosho.

No comments:

Powered by Blogger.