Header Ads

THAILAND YAMSHITAKI RASMI WAZIRI MKUU WAKE ‘YINGLUCK SHINAWATRA’ KWA TUHUMA ZA UFISADI

Yingluck Shinawatra
Yingluck Shinawatra
Tume ya kupambana na ufisadi nchini Thailand imemshitaki rasmi waziri mkuu aliyeondolewa madarakani Yingluck Shinawatra kwa madai ya kupuuza jukumu lake katika usimamizi wa mpango uliokosolewa vikali wa kutoa ruzuku ya mchele.
Hatua hiyo imekuja baada ya mahakama ya katiba kumuondoa madarakani waziri mkuu huyo ambaye anatuhumiwa kwa kuruhusu mpango huo wa mchele uliokuwa sera muhimu katika utawala wake kuendelea licha ya kushauriwa kwamba ulikuwa ukitumiwa vibaya na kuzongwa na ufisadi.
Uamuzi huo unamaana kuwa mwanamama YingLuck atakabiliwa na kura ya kumng’oa madarakani katika baraza la seneti ikiwa theluthi tano ya kura zitaunga mkono uamuzi wa kumtia hatiani na anaweza kuzuiwa kushiriki katika masuala ya  siasa kwa miaka mitano.

No comments:

Powered by Blogger.