Header Ads

TASAF YAWAFUNDA WATAALAM WA KISEKTA JUU YA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI-PSSN

Mkurugenzi mtendaji wa TASAF, bwana Ladislaus Mwamanga amesema utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya Masikini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii nchini TASAF utasisimua shughuli za maendeleo kwenye maeneo mbalimbali ya nchi ambako utatekelezwa na hivyo kuwa chachu ya maendeleo na  kuondoa kero zinazowakabili wananchi hususani suala la umasikini.

Bwana Mwamanga amesema hayo jiji Dar es salaam alipofungua  warsha ya wataalamu wa kisekta kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ambao sekta zao zinahusika kwa namna moja au nyingine katika utekelezaji wa shughuli za TASAF kwenye maeneo yao.

Mkurugenzi mtendaji huyo wa TASAF amesema kwa kiwango kikubwa  utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya masikini umeanza kutekelezwa kwa mafanikio ambapo mwelekeo umeonyesha kuwa maeneo ambako Mpango huo umefanyiwa majaribio kumekuwa na mafanikio ya kujivunia hususani katika sekta za Elimu, Afya, na hata Lishe kwa kaya ambazo hapo awali hazikuwa na uhakika wa kupata lishe.

Hata hivyo, bwana Mwamanga amewataka wataalamu hao wa kisekta kutumia utaalamu wao ipasavyo ili waweze kuielewa dhana nzima ya Mpango wa kunusuru kaya masikini na kuhakikisha kuwa wanawawezesha wananchi hususani walioko katika kaya masikini ili waweze kuondokana na umasikini.

Mkurugenzi huyo mtendaji wa TASAF pia ametaka mkakati maalum uwekwe ili kuhakikisha kuwa huduma muhimu hususani za upatikanaji wa elimu na Afya  unakuwapo  ili walengwa wa mpango huo waweze kunufaika nazo.

Zifuatazo ni picha za ufunguzi wa warsha hiyo ya wataalamu wa kisekta iliyofanyika leo katika hoteli ya Golden Jubelee jijijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga (aliyesimama) akifungua warsha ya wataalam wa  Kisekta (hawapo pichani) jijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi wa Miradi wa TASAF Bwana Amadeus Kamagenge (aliyesimama)akitoa maelezo ya utangulizi katika warsha ya wataalamu wa kisekta   jijini Dar es salaam katikati ni Mkurugenzi mtendaji wa TASAF Ladislaus Mwamanga  na kushoto kwake ni mkurugenzi wa uratibu wa TASAF  Alphonse Kyariga.
 Mkurugnezi wa uratibu wa shughuli za Muungano katika Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Bwana Issan Ibrahim Mohmond (aliyevaa  koti )akimsikiliza mkurugenzi mtendaji wa TASAF, Ladislaus Mwamanga (hayupo pichani) alipofungua warsha ya wataalam wa kisekta jijijin Dar es salaam  mbele yake ni Mkurugenzi wa Ukaguzi wa TASAF Bwana Christopher Sanga.
Baadhi ya washiriki wa warsha ya wataalamu wa Kisekta wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa warsha ya wataalam wa kisekta iliyotolewa na mkurugenzi mtendaji wa TASAF Ladislaus Mwamanga(hayupo pichani).
Baadhi ya washiriki wa warsha ya wataalamu wa Kisekta wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa warsha ya wataalam wa kisekta iliyotolewa na mkurugenzi mtendaji wa TASAF Ladislaus Mwamanga(hayupo pichani).
Mtaalamu wa teknolojia ya habari na mawasiliano ICT wa TASAF Bwana Peter Luanda(wa kwanza  kushoto)na meneja wa uhawilishaji wa fedha Bwana Omar Malilo (mwenye miwani katikati)wakiwa katika warsha ya wataalamu wa kisekta iliyoandaliwa na TASAF jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Ladislaus Mwamanga (aliyeketi katikati )akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha ya wataalam wa kisekta  iliyoandaliwa na kwa lengo la kuwaelewesha namna ya utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya masikini nchini unaoratibiwa na Mfukowa Maendeleo ya Jamii TASAF.

No comments:

Powered by Blogger.