Header Ads

RAIS WA ZANZIBAR DK ALI MOHD SHEIN AFUNGUA KATUO CHA KURUSHIA MATANGAZO YA DIJITALI ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akikata Utepe kuonyesha Ufunguzi wa Kituo Kikuu cha Kurushia Matangazo ya Dijitall huko Rahaleo Mkoa wa Mjini Unguja.ikiwa ni Shmra shamra za Kuadhimisha Sherehe za Kutimia Miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Kituo kikuu cha Mtambo wa Kurushia Matangazo ya Dijitall kilichofunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi huko Rahaleo Mkoa wa Mjini Unguja.ikiwa ni Shmra shamra za Kuadhimisha Sherehe za Kutimia Miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein wapili kushoto akipata maelezo mafupi kwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Agape Association LTD Dr Vernon Fernandes wakwanza kuli kuhusiana na Chanall za Dijitall zinavyofanya kazi,baada ya Rais kufungua Kituo Kikuu cha Kurushia matangazo ya Dijitall hapo Rahaleo Mjini Zanzibar.wapili kulia ni Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk.
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein katikati akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo na Mainjinia wa Ujenzi wa Kituo Kikuu cha Kurushia matangazo ya Dijitall hapo Rahaleo Mjini Zanzibar.PICHA NA YUSSUF SIMAI -MAELEZO ZANZIBAR.
…………………………………………………….
Na Khadija Khamis –Maelezo Zanzibar   

 SHIRIKA la Utangazaji  Zanzibar ZBC limetakiwa kuhakikisha kwamba linafanyakazi kwa ufanisi mkubwa kulingana na mfumo uliopo hivi sasa.
Alisema kuwa wafanyakazi wa shirika hilo wameonakana wakifanya kazi kimazowea tu bila kufuata taratibu za kikazi.  

Hayo yameelezwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dkt Ali Mohammed Shein katika Uzinduzi wa Miundombinu ya Dijitali na Jengo la Studio ya Kisasa Alisema kuwa kubadilika kwa watendaji kazi ni suala la lazima kutokana na mabadiliko makubwa yalioko duniani .

Dkt Shein alisema kuwa ZBC wananchi wengi wanapiga kelele juu ya utendaji wa wafanyakazi wa ZBC kutokana na  vipindi vyao kutoridhisha na kukatika katika kwa matangazo yao zaidi wakati wa taarifa ya habari.

Alisema kuwa Zanzibar inaheshima yakekatika masuala ya Utangazaji kwani Redio nyingi za Nje zinawatangazaji kutoka Zanzibar ambao ni mahiri katika masuala ya Utangazaji.

No comments:

Powered by Blogger.