Header Ads

Harambee ya ujenzi wa Kanisa la KKKT mkoani Rukwa – yafana

1
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, akijadiliana jambo na Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa (katikati) na Askofu Ambele Mwaipopo wa Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, wakati wa harambee ya ujenzi wa Kanisa la KKKT mkoani Rukwa. Katika harambee hiyo Nyalandu, aliyekuwa mgeni rasmi alichangia sh. Milioni 100. Harambee hiyo ilifanyika jana usiku katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam.
2 3
ASKOFU Ambele Mwaipopo wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Ziwa Tanganyika, akimkabidhi zawadi mbalimbali zilizotolewa na waumini wa kanisa hilo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, wakati wa harambee ya kuchangia kanisa.
4
Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, akimkabidhi zawadi maalumu aliyopewa na Papa Francis XIV, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, ikiwa ni ishara ya kuthamini mchango wa sh. Milioni 100 alioutoa kuchangia ujenzi wa kanisa mjini Sumbawanga.

No comments:

Powered by Blogger.