Header Ads

RIDHIWANI KIKWETE AAHIDI KUTATUA TATIZO LA UMEME, MAJI KIWANGWA,CHALINZE

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete (kulia), akipata maelezo kutoka kwa Msimamizi wa ujenzi kutoka Kambi ya Mzinga ya JWTZ, Aloyce Mayunga (kushoto) alipokwenda kukagua ujenzi wa maabara ya Shule ya Sekondari ya Kiwangwa wakati wa ziara ya kikazi ya katika Kata ya Kiwangwa, wilayani Chalinze, Pwani leo.Aliwataka wajenzi hao kujenga maabara hayo kwa kuzingatia viwango. Katikati ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Bagamoyo, Saleh Mpimbwi.
 Ridhiwani Kikwete akizungumza na wakandarasi kutoka Kambi ya Mzinga ya JWTZ wanaojenga maabara ya Shule ya Sekondari ya Kiwangwa wakati wa ziara ya kuagua miradi ya maendeleo na kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa mbunge miezi sita iliyopita. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Ridhiwani akinyoosha juu kadi ya Chadema aliyokabidhiwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa  Chadema Kijiji cha Masugulu ambaye amehamia CCM katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mwitemo Kata ya Kiwangwa leo
 Ridhiwani akihutubia wananchi  katika Kijiji cha Mwitemo
 Sehemu ya akina mama wakisikiliza kwa makini wakati Ridhiwani Kikwete akihutubia katika Kitongoji cha Magogoni, Kijiji cha Msinune, Kata ya Kiwangwa.
 Ridhiwani Kikwete akihutubia wananchi katika Kijiji cha Msinune, Kata ya Kiwangwa.

No comments:

Powered by Blogger.