MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO AIWAKILISHA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA PILI WA KIMATAIFA KUHUSU LISHE NA VIRUTUBISHO JIJINI ROME, ITALIA NOVEMBA 21, 2014

Papa Francis, akihutubia wakati wa mkutano huo....

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akihutubia Mkutano wa pili wa Kimataifa kuhusu Lishe na Virutubisho
(ICN2) uliofanyika katika ukumbi wa Makao Makuu ya Shirika la Kilimo na
Chakula la Umoja wa Mataifa (FAO) jijini Rome, Italia juzi Novemba 19,
2014.

Mheshimiwa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akifuatilia hotuba mbalimbali za viongozi walioshiriki katika
Mkutano huo wa ICN2. Kulia ni Mfalme Letsie III wa Lesotho.

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mpango Maalum wa
Chakula Duniani (WFP) Ethria Cousin (kulia) na Balozi Wilfred Ngirwa
wakati wa mkutano huo wa ICN2, uliofanyika juzi Novemba 19, 2014, Jijini
Rome Italy.

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akijadiliana jambo na baadhi ya wajumbe kutoka Tanzania wakati wa
mkutano huo wa ICN2 (kushoto) ni Balozi wa Tanzania nchini Italia, James
Nsekela na Msaidizi wa Rais katika Masuala ya Lishe Dkt. Wilbald Lorri.

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akijadiliana jambo na baadhi ya wajumbe kutoka Tanzania wakati wa
mkutano huo wa ICN2 (kushoto) ni Balozi wa Tanzania nchini Italia, James
Nsekela na Balozi Wilfred Ngirwa (kulia).

Mheshimiwa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal (katikati) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mtendaji wa FAO
Jose Graziano da Silva, wakati alipomtembea ofisini kwake na kufanya
naye mazungmzo, juzi Novemba 19, 2014. Kushoto ni Waziri wa Afya na
Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashid. Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
---
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA MAAKAMU WA RAIS

Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal
Novemba 19, 2014 ameiwakilisha Tanzania katika Mkutano wa Pili wa
Kimataifa kuhusu Lishe na Virutubisho uliofanyika katika Makao Makuu ya
Shirika la Kilimo na Chakula la
Umoja wa Mataifa (FAO) jijini Rome Italia.
Mkutano
huu umefanyika ikiwa ni miaka 22 baada ya mkutano wa kwanza maarufu kwa
jina la ICN1 kufanyika katika jiji la Rome na kuazimia kuwa, upo
umuhimu wa kuhakikisha binadamu wanapata Lishe bora yenye virutubisho
ili kusadia kujenga afya ya binadamu duniani. Mkutano huu wa pili pia
umeandaliwa kwa pamoja na Shirika la Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO)
pamoja na Shirika la Afya Duniani (WHO).
No comments:
Post a Comment