Header Ads

KAMPUNI YA PAN AFRICAN ENERGY YATOA MSAADA WA MIFUKO 1500 YA SARUJI KWA WILAYA YA KILWA

Meneja wa Uwajibikaji na Huduma za Jamii wa Kampuni ya uchimbaji wa gesi ya Pan African Energy, Andrew Kashangaki (kwanza kushoto) akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilwa Peter Malekela (kulia) msaada wa saruji 1,500 yenye thamani ya shilingi milioni 18 kwa halmashauri ya wilaya ya Kilwa, Lindi ili kuwezesha ujenzi wa maabala 59 katika shule zake za sekondari zipatazo 24. Pembeni wanaoshuhudia ni viongozi wa halmashauri hiyo na wafanyakazi wa Kampuni ya uchimbaji wa gesi ya Pan African Energy. Makabidhiano hayo yalifanyika mwanzoni mwa wiki Novemba 17, 2014 katika kiwanda cha Saruji cha Kilwa, Lindi.
Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya Peter Amosi Malekela akizungumza machache.
Waandishi wa habari wakifanya mahojiano na mwalimu wa masomo ya sayansi wa shule ya sekondari Mtanda ambapo uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa na viongozi toka kampuni ya  Pan African Energy (T) Ltd.
Moja ya Maabala inayojengwa kwa msaada wa Pan African Energy (T) Ltd.

No comments:

Powered by Blogger.