PUSH MOBILE, UN , WIZARA KUKABILI EBOLA
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati)
na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Push Mobile, Freddie Manento (kushoto)
wakitiliana saini makubaliano ya ushirikiano wa kukabiliana na ugonjwa
wa ebola kwa kutoa elimu kwa jamii kupitia ujumbe mfupi maneno katika
hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za Mratibu mkazi wa mashirika ya
Umoja wa Mataifa jijini Dar. Anayeshuhudia tukio hilo ni Mwakilishi wa
UNICEF Tanzania, Dkt. Jama Gulaid.(Picha na Umoja wa Mataifa).
KAMPUNI
ya simu ya Push Mobile imetiliana saini na serikali ya Tanzania na
Umoja wa Mataifa (UN) ya kuwafikia watu milioni 10 ikiwahabarisha kuhusu
ugonjwa hatari wa ebola.
Kwa
mujibu wa taarifa ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa mjini hapa kampuni
hiyo ya simu imesema kupitia ushirikiano huo kampuni hiyo ya simu
itaunga mkono juhudi za serikali ya Tanzania na Umoja wa Mataifa wa
kutoa elimu dhidi ya ugonjwa huo ujumbe mfupi utakaoelezea ugonjwa wa
ebola.
Kama
sehemu ya makubaliano, Push Mobile , UN, serikali na wadau wake watatoa
taarifa kuhusu ugonjwa huo wanapohitajika. Watanzania wanaweza kupata
habari za ugonjwa huo kwa kuandika neno EBOLA kwenye namba 15774 na
kupata taarifa za ugonjwa huo bure bila kutozwa gharama.
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Push Mobile, Freddie Manento wakionyesha hati za
makubaliano ya ushirikiano huo.
Wakitia
saini Ofisa Mtendaji Mkuu wa Push Mobile, Freddie Manento amesema
kwamba kama Ujumbe mfupi unaweza kuokoa maisha kampuni yake iko tayari
kushiriki katika kampeni hiyo.
No comments:
Post a Comment