REDIO YA JAMII MKOANI YAZINDULIWA KWA MBWEMBWE ZA MAPINDUZI
Katibu
Mtendaji wa Tume ya Utangazaji Zanzibar (ZBC), Chande Omar (kulia)
akifafanua jambo kwa Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na
mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini,
Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) kabla ya kuanza kwa sherehe za
uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani iliyopo Kusini Pemba. Katikati ni Afisa
Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Bw. Al Amin Yusuph na kushoto ni
Mke wa Mratibu Mkazi wa UN Tanzania, Bi. Fainula Kurji-Rodriguez.
Meneja
wa Redio Jamii Mkoani jimbo la Mkanyageni Mkoani Kusini Pemba, Bw. Ali
Abbas akisoma risala ya kituo chake mbele ya mgeni rasmi Waziri wa
Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto visiwani
Zanzibar, Mh. Zainabu Omari Mohammed (hayupo pichani) wakati wa sherehe
za uzinduzi wa kituo hicho cha redio.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo visiwani
Zanzibar, Juma Yakufi akisoma hotuba kwa niaba ya Waziri mwenye dhamani
ya wizara hiyo wakati wa sherehe za uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani jimbo
la Mkanyageni mkoani Kusini Pemba uliofanyika mwishoni mwa wiki
visiwani humo.
Mkuu
wa Wilaya ya Mkoani Kusini Pemba, Hemedi Selemani akitoa neno la
shukrani wakazi wa mkoani jimbo la Mkanyageni pamoja na wageni waalikwa
kwenye sherehe za uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani ya Kusini Pemba
uliofanyika mwishoni mwa wiki.
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika
la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez
akizungumza kwenye uzinduzi wa Redio Jamii Mkoani ya Kusini Pemba
uliofanyika mwishoni mwa wiki.
No comments:
Post a Comment