Header Ads

WATANZANIA WATAKIWA KUTODANGANYWA KUHUSU MCHAKATO WA KATIBA

 Na Benedict Liwenga, MAELEZO-Dodoma.

 
MJUMBE wa Bunge Maalum la Katiba ambaye pia ni Mwenyekiti wa TCD Mhe. John Cheyo amewataka Watanzania kutodanganywa kuhusiana na mchakato mzima wa kusaka Katiba Mpya.
 
Kauli hiyo imetolewa leo na Mhe. Cheyo wakati alipokuwa akifanya mahojiano katika kipindi cha asubuhi cha Jambo kinachorushwa na Televisheni ya Shirika la Habari Tanzania (TBC).
 
Mhe. Cheyo amesema kuwa ni vema viongozi kuacha kusema uwogo na kuwa waungwana katika mchakato wa kutafuta Katiba Mpya kwani si vema kuitakia Tanzania mabaya bali ni kutaka mchakato huo wa Katiba uendelee kwa amani.
 
Ameongeza kuwa Taifa la Tanzania linahitaji kuwa Taifa lenye nguvu kwani amani haiwezu kuwekewa thamani kwa vurugu, hivyo ametaka amani iliyopo nchini ilindwe na kuepuka kudanganywa na baadhi ya watu wasiokuwa na nia njema na nchi.
 
Mhe. Cheyo ameshangazwa kwa kitendo cha viongozi wa UKAWA kutoweka ajenda ya kurudi ndani ya Bunge hilo wala kuzungumzia kuhusu suala hilo la kurudi ndani, bali wamekuwa wakitaka wajumbe wengine walioko ndani watoke kwa kusema kuwa bunge hilo sio halali.
 
“Nawashangaa UKAWA kwa kutoweka ajenda ya kurudi ndani ya Bunge hili Maalum la Katiba na badala yake wao wanaweka ajenda ya kutoka ndani ya bunge hili tena kwa nguvu”, alisema Mhe. Cheyo.
 
Aidha, Mhe. Cheyo amewataka vijana nchini wawe na mshikamano na kuepuka kudanganywa na viongozi kwa kuambiwa mambo yenye uwongo huku akisisitiza kuwa Rais aliyeko sasa hivi ana nia njema ya kuipatia nchi Katiba iliyo bora na yenye kumfaa kila Mtanzania.

No comments:

Powered by Blogger.