UMOJA WA MATAIFA WATAKA CHANZO CHA SIASA KALI ZINAZOLETEA MIGOGORO ZICHUNGUZWE
Makamu
Mwenyekiti wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Joseph Masasi akitoa
neno la ukaribisho kwa mgeni rasmi Mh. Seif Rashid (wa pili kulia).
Kutoka kushoto ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na
mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini,
Alvaro Rodriguez, Kamishna wa Ustawi wa Jamii, Bw. Dunford Makala,
Balozi wa Uturuki nchini, Mh. Ali Davutoglu.
Mgeni
rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Amani, Waziri wa Afya
na Ustawi wa Jamii, Mh. Seif Rashid, akisoma hotuba kwenye maadhimisho
ya siku ya kimataifa ya amani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi
Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akisoma
ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-Moon kwenye
maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani duniani.
Mratibu
Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez
akipongezwa na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mh. Ali Davutoglu
baada ya kusoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Mkurugenzi
Mtendaji wa shirika la UNDER THE SAME SUN, Vicky Ntetema akisoma risala
yake kwa mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya
amani iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mufti Sheikh Ismail Habibu Makusanya, akizungumza kwenye maadhimisho
hayo ambapo alilaani vikali mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi
(Albinizim) na kusema kuwa watu wote wanaoshiriki katika mauaji hayo
kamwe hawatoiona Pepo ya Mwenyezi Mungu.
Balozi
wa Uturuki nchini Tanzania, Mh. Ali Davutoglu akisoma ujumbe kwa niaba
wa umoja wa mabalozi kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya amani
duniani.
Baadhi ya wadau kutoka taasisi na asasi mbalimbali nchini walioshiriki kwenye maadhimisho hayo.
Katibu
Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini Tanzania
(THBUB), Bi. Mary Massay akitoa nasaha kutoka kwa Tume hiyo, ambapo
alitoa rai kwa mtu yeyote yule ambaye ana malalamiko au matatizo katika
Haki za Binadamu anakaribishwa kwenye tume hiyo kwa ajili kupata msaada
wa kisheria.
No comments:
Post a Comment