Tutengeneze Katiba inayolenga kutatua matatizo ya wananchi wetu kwa miaka 50 ijayo: Prof. Mwandosya.
Mjumbe
wa Bunge Maalum, Mhe. Prof. Mark Mwandosya akichangia mjadala wa ndani
ya Bunge Maalum kujadili taarifa za kamati za bunge hilo
zilizowasilishwa wiki iliyopita kwa ajili ya kuandika Katiba
inayopendekezwa.(Picha na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma)
Na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma.
MJUMBE wa Bunge Maalum la Katiba Mhe. Prof. Mark
Mwandosya ameeleza kuwa mpaka ifikapo mwaka 2055 Tanzania itakuwa imeachana na
umaskini katika nchi ya uchumi wa kwanza endapo kutakuwa na dhamira ya dhati hususani
kuwa kuandika Katiba yenye kuleta nafuu kwa watanzania kwani kila kitu kwa
Waafrika kinawezekana pasipo kuwa na Wazungu.
Prof. Mwandosya alisema hayo jana wakati akichangia
mjadala wa katiba ndani ya Bunge Maalum, ambapo alisisitiza umuhimu wa kuwa na
katiba itakayozingatia vipaumbele ambavyo vinaweza kumkwamua mwananchi wa
kawaida kuondokana na umasikini na kuliinua Taifa kiuchumi.
Mhe. Mwandosya amesema kuwa kuhusu changamoto na kero
zinazohusu mambo ya Muungano, katiba imejaribu kuzizingatia karibia zote, huku
akieleza kuwa hali ya Muungano ni imara na itaendelea kuwa imara.
No comments:
Post a Comment